Habari njema
Tubuni
Ufalme wa yesu
Yesu na ufufuo
Yesu ndiye kristo
Mche mungu
Ubatizo wa maji mengi
Yesu ni bwana
Watumishi Yesu
|
" Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia."( Math. 3:2).
Hiyo ni habari njema ambayo yesu kristo aliwahubiri wenye dhambi kondoo wa Israeli waliopotea kumrudia muumba wao. Habari hiyo njema kila siku iko hivyo hivyo kwa mtu anayejifahamu yeye ni mwenye dhambi na anayeishi maisha ya dhambi ya kuzivunja amri kumi za mungu ikiwemo usiibe , kupokea rushwa kufanya ufisadi, kuvuta madawa ya kulevya au kuuza.n.k.
Ukweli leo kama unasoma mahubiri haya ni wakati wako kubadilika usifanye mgumu moyo wako unahitajika kutubu kwa jina la yesu nakuamini yesu alisulubiwa kwa ajili ya dhambi zako na laana zako zipate kuondolewa na baada ya siku tatu alifufuka akupe maisha mapya huru mbali na dhambi kama walivyotabiri manabii wa kale ili kwa njia ya yeye upate kupatanishwa na mungu na kupewa haki yake ya kuwa mwana mbele za mungu kwa kutupa msaidizi roho mtakatifu wa kutuongoza na kutia ktk kweli yote. Yesu alitoa maisha yake apate kukuokoa kutoka ktk maisha ya rushwa , ulevi, ukahaba, uzinzi, uuaji, wizi, ujambazi n.k na laana zilitokana na kuishi maisha hayo kama magonjwa mfano ugumba au utasa, Blood pressure, upofu(B.P),umaskini.
Hayo maisha ya dhambi na laana zinakutesa ni kwa sababu ufalme wa mungu haumo ndani yako dhambi ndiyo inayotawala ndani yako wala si mungu na ufalme wake ambao ni wa haki na baraka lakini leo usomapo mahubiri haya ufalme umekaribia ukiukaribisha unaingia moyoni mwako na mungu anapata haki ya kutawala kupitia huo na dhambi inakuwa haitawali tena maisha yako. Ili Yesu aingie moyoni mwako lazima uokoke."; bofya Kuokoka
<||---kurudi nyuma <<<||>>> kuendelea mbele---||>
|